Ijue Parokia
Malengo ya parokia
Kwa sasa viongozi wa Parokia ya Mwenyeheri Vincenza Maria Poloni wataendelea kuelekeza nguvu zao katika kuwahamasisha wakristo ambao kwa namna moja au nyingine kwa sasa hawajihusishi kushiriki shughuli za kanisa, kuwafuatilia kwa upendo wakristo wa parokia ambao wamelegalega na kuwasaidia waweze kumrudia Kristu. Kuhakikisha kuwa taratibu zote za uendeshaji wa shughuli za kitume hapa parokia ya Utatu Mtakatifu Changanyikeni zinaboreshwa na zina msaidia Mkristu azidi kuimarika katika Imani yake asilegee kamwe, Kristu amkute angali anakesha (LK. 21:36; Mk 13:33; Ufu 6:17).
Parokia Inategemea kutekeleza shughuli mbalimbali katika mfumo wa mipango ya muda mfupi na muda mrefu kulingana na upatikanaji wa fedha na rasilimali mbalimbali za ujenzi wa Kanisa
- Kuanzisha mbinu/mkakati maalum kwa ajili ya kuinua kiwango cha kutegemeza kanisa hasa sadaka na zaka, pamoja na kuhimiza majitoleo ya wakristo binafsi au familia
- Kuongeza jitihada hasa kuwafikia wale waamini ambao wana vizuizi mbalimbali dhidi ya sakramenti za kanisa na kuwasaidia kuzipokea kukuza Uchaji wa Mungu ndani mwao
- Kuanzisha/kuendeleza semina mbalimbali za kiroho ili kuwawezesha waamini kukua katika kuielewa vema Imani Katoliki ipasavyo na kukuza miito.
- Kuendeleza semina za kujitoa na kumtolea Mungu (Malaki 3:8-12)
- Kuanzisha huduma ya Bimaya Afya na ya Maisha kwa Wakristo Wetu.
- Kumalizia ujenzi wa Kanisa letu la Parokia ya Mwenyeheri Vincenza Maria Poloni
- Ujenzi wa Chuo cha ufundi
- Ujenzi wa nyumba ya Masista
- Kuanzisha shule ya Chekechea
- Ujenzi wa Zahanati
- Kuanzisha miradi mingine ya maendeleo katika Parokia eg. Duka la Parokia
- Ujenzi wa Groto ya Bikira Maria
- Groto ya Msalaba Mtakatifu
- Groto ya Moyo Mtakatifu
- Kuweka ukuta kuzungukia eneo la kanisa la Parokia ya Mwenyeheri Vincenza Maria Poloni.
- Kuongeza ghorofa kwenye nyumba ya mapadre kwa ajili ya huduma zingine kadiri itakavyoonekana inafaa kwa muda muafaka kuongezea kipato Parokia.